Monday, November 14, 2011

Viwawa kigango cha kwa MROMBO watembelea viwawa njiro

Matukio ktk picha
Hawa juu ndo viwawa Uongozi wa Viwawa njiro Tunawapongeza sana kwa matembezi yenu bora katika parokia yetu tumejifunza mengi kutoka kwenu...Asante sana.

Saturday, October 22, 2011

Kongamano la kijimbo Arusha mwaka 2012 SIKU 5


Leo 22/10/2011 kulikuwa na kikao cha Viongozi wa Viwawa Parokiani St.theresia Wajumbe walipendekeza siku ya kongamano la kijimbo na kufikia maamuzi kuwa kifanyike mwezi wa sita mwakani na kila mshiriki kuchangia kiasi cha sh 35,000 Tsh na kongamano litakuwepo mwezi wa sita kati 15.06.2012 up 24.06.2012 mwaka kesho,Na slogani ya kongamano kutoka katika muhubiri 12;1 au zaburi 199:9 Katika pesa hiyo ya 35,000 kila mshiliki hatapatiwa TISHETI YA KONGAMANO,Kongamano litakuwa la siku TANO kuanzia jumatano,LITAKUWA KONGAMANO Bora sana.

Thursday, October 20, 2011

Vijana jitaabisheni kuzifahamu Sakramenti za Kanisa: mwanzo, uponyaji, ushirika na huduma!

Mpendwa kijana, uchambuzi wetu wa Katekismu ya Vijana, YOUCAT, unatuingiza katika kuzichanganua Sakramenti Saba za Kanisa.
Kwa ujumla Sakramenti za Kanisa zinaweza kupangwa katika makundi makuu matatu. Kundi la kwanza ni la Sakramenti za Mwanzo, ambazo zinamwingiza mtu katika kupokea imani. Sakramenti za kundi hili ni tatu: Ubatizo, Kipaimara na Ekaristi Takatifu. Kundi la pili lina Sakramenti za Uponyaji: yaani Kitubio na Mpako wa Wagonjwa. Na kundi la tatu ni la Sakramenti za Ushirika na Huduma: hizi ni sakramenti ya Ndoa na Madaraja Matakatifu.
SAKRAMENTI YA UBATIZO ni sakramenti ya msingi na ufunguo wa sakramenti zote, ni agano ambalo mtu hanabudi kulikubali; ni njia ya kutoka katika ufamle wa mauti kuingia uzimani; na ni mwanzo wa muungano dumifu na Mungu. Ubatizo unaweza kufanyika kwa kumzamisha mtu mara tatu ndani ya maji au kwa kummwagiliwa maji kichwani mara tatu huku kukitamkwa “F… nakubatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.” Maji ya Ubatizo yanawakilisha maisha mapya na kutakatifuzwa katika Kristo. Ibada ya ubatizo hufungwa kwa kupakwa mafuta matakatifu, vazi jeupe na mshumaa wa ubatizo. Ubatizo unatolewa kwa mtu yeyote ambaye hajabatizwa.
Hitaji la lazima ili kubatizwa ni imani ambayo mtu anaiungama hadharani wakati wa ubatizo. Ubatizo hutolewa pia kwa watoto wachanga ambapo ungamo la imani hufanywa na wazazi kwa niaba ya watoto hao. Ukweli ni kwamba kabla mtu hajaitikiwa wito wa kubatizwa Mungu tayari amekwisha mkubali kuwa miongoni mwa watoto wake.
Na hivyo ubatizo ni neema, ni zawadi tusiyoistahili toka kwa Mungu. Kukubali Ubatizo wa mtoto mchanga kwa wazazi waamini ni tendo la upendo na matashi mema ya kumnasua toka dhambi ya asili na nguvu ya mauti. Mtu yeyote anapobatizwa anakuwa mshirika wa Mwili wa Kristo, kaka na dada wa Mwokozi, na mwana wa Mungu.
Kwa mtu yeyote aliyepokea Injili na kufahamu kuwa Kristo ni “njia, na kweli na uzima” (Yoh 14:6), Ubatizo ni njia pekee ya kwenda kwa Mungu na ya wokovu. Hata hivyo, kwa vile Kristo alikufa kwa ajili ya watu wote, wale wote ambao hawajapata nafasi ya kujifunza kumhusu Kristo na imani lakini wanamtafuta Mungu kwa dhamiri zao wanapata wokovu kwa ubatizo wa tamaa.
Kwa kawaida, Sakramenti ya Ubatizo huadhimishwa na Askofu, Padre au Shemesi. Lakini katika hatari ya kifo kila mkristo au mtu yeyote (hata asiye mkristo) naweza kubatiza kwa kutumia maji na kutamka maneno ya ubatizo: “F. Nakubatiza kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu”. Anayebatiza hana budi kuwa na nia ya kutenda kile kinachofanywa na Kanisa linapobatiza.
Katika Ubatizo mtu hupokea jina jipya ikionesha kwamba Mungu mwenyewe amemuita kwa jina, anamfahamu, na hivyo ni wake. (Is 43:1). Mkristo huchagua jina la watakatifu ili kijipatia mfano wa kuigwa na kupata msaidizi, rafiki aliye kwa Mungu.
SAKRAMENTI YA KIPAIMARA inakamilisha ubatizo kwa kumpatia mwimarishwa zawadi ya Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono; na kwa kupakwa mafuta matakatifu ya Krisma anapata nguvu ya kutoa ushuhuda wa upendo na uwezo wa Mungu kwa maneno na matendo. Mwimarishwa anakuwa mshirika kamili na mwajibikaji wa Kanisa Katoliki.
Katika Agano la Kale, watu walisubiri ujio wa Roho Mtakatifu juu ya Masiha. Na katika maisha yake, Kristo ameonesha kuwa na Roho wa upendo na muungano kamilifu na Baba. Huyu ndiye Roho aliyesubiriwa katika Agano la Kale, na ambaye Kristo aliwaahidia wafuasi wake; ndiye aliyewashukia wafuasi wake siku ya Pentekoste, na anayemshukia kila mmoja apateye Kipaimara.
Kinachofanyika wakati wa Kipaimara ni kwamba roho ya mkristo mbatizwa inapata muhuri usiofutika na unaomtambulisha mtu kuwa mkristo daima. Paji la Roho Mtakatifu linamwimarisha mtu kuwa shuhuda wa Kristo kwa maneno na matendo kupitia neema ya ubatizo.
Kipaimara kinaweza tu kutolewa kwa Mkristo Mkatoliki aliyebatizwa na aliye katika hali ya neema, yaani asiwe katika dhambi ya mauti. Kama mtu ametengana na Mungu kwa dhambi kubwa anapaswa kujipatanisha naye kwa kupokea Sakramenti ya kitubio. Sakramenti ya Kitubio inahitajika pia katika mazingira yote ambapo mtu anahitaji kujipatanisha na nafsi yake, na watu wengine, na Mungu, na kumkaribia Mungu hata kama hajatenda dhambi ya mauti.
Mwadhimishaji wa kawaida wa Sakramenti ya Kipaimara ni ASKOFU. Hata hivyo kama kuna sababu nzito na za lazima, Askofu anaweza kumruhusu padre atoe Kipaimara. Kunapokuwa na hatari ya kifo, padre yeyote anaweza kutoa kipaimara.
Kwa leo mpendwa kijana, naomba tukunje jamvi letu ili tuweze kujipatia muda wa kucheua haya tuliyopokea. Uchambuzi wetu wa Sakramenti saba za kanisa utaendelea wiki ijayo, siku na wakati kama huu. Nikikutakia kila jema, kutoka hapa Vatican, ni mtumishi wako, Padre Flavian Kassala.SOURCE kutokahttp://www.radiovaticana.org/EN3/articolo.asp?c=504225

Nyaraka za siri toka Vatican kuoneshwa hadharani, Februari, 2012 mjini Roma

 chanzo cha HABARI>>>www.radiovaticana.org
Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican, Jumanne, tarehe 5 Julai, 2011 ameongoza jopo la viongozi waandamizi kutoka Vatican wakati wa kuwasilisha mkakati wa Vatican kushiriki katika onesho la Kumbu kumbu za Nyaraka za Siri za Vatican, litakalofanyika kwenye Jumba la Makumbusho la Jiji la Roma, hapo mwezi Februari, 2012.

Hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa nyaraka za siri kutoka nje ya Vatican kwa ajili ya onesha la hadhara. Mkutano na waandishi wa Habari umehudhuriwa pia na Mstahiki Meya wa Jiji la Roma, Giovanni Alemanno na ujumbe wake.

Akizungumza na waandishi wa Habari, Kardinali Bertone anasema kwamba, tukio hili si la kawaida kwani linafanyika nje ya kuta za Vatican na litafanyika kwenye Jumba la Makumbusho la Roma, kitovu cha Jiji la Roma na utajiri wake unaofumbata uhusiano wa pekee na Vatican miaka nenda miaka rudi. Changamoto iliyokuwa mbele yao ni ile ya kuhakikisha kwamba, utajiri mkubwa, uzoefu na mang'amuzi yaliyoko kwenye nyaraka za siri za Vatican yanakwenda sanjari na matarajio ya Jiji la Roma.

Kwa upande wake, Kardinali Raffaele Farina, Mkutubi mkuu wa Vatican, alifafanua kwamba, nyaraka za kipapa zinazohifadhiwa kwenye Jumba la Kumbu kumbu za Nyaraka za Siri za Vatican ni muhimu sana katika maisha na utume wa Kanisa zima. Kwa mara ya kwanza, watu mbali mbali wanaweza kuzisoma nyaraka hizi ili kujichotea utajiri uliomo.

Askofu Sergio Pagano, Katibu mkuu wa Nyaraka za Siri za Vatican anasema, onesho hili linapania kutoa mwanga na uelewa mpana zaidi kuhusu asili na yaliyomo kwenye nyaraka hizi za siri zinazohifadhiwa katika Kumbu kumbu za Siri za Vatican, ndiyo maana onesho hili limepewa jina katika lugha ya Kilatini "Lux in Arcana" "Mwanga katika bahari". Kuna mammilioni ya nyaraka mbali mbali za Kanisa kutoka Vatican, kati ya hizo zote, Maktaba ya Vatican imeamua kuonesha nyaraka mia moja kwa wakati huu. Hali hii inaonesha kazi kubwa inayopaswa kufanywa ili kuwezesha umati mkubwa kushuhudia na kujisomea nyaraka hizi za Siri kutoka Vatican.

Kati ya nyaraka zitakazooneshwa ni ile ya Baba Mtakatifu Gregory wa Saba aliyeishi kunako mwaka 1073 hadi 1085; Barua ya Baba Mtakatifu Clementi wa Saba kwa Mfalme Henri wa nane kuhusu mgogoro wa ndoa, iliyoandikwa kunako mwaka 1530. Bila shaka wengi wangependa kufahamu kilichoandikwa na Kanisa wakati wa mashitaka ya Galileo Galilei kunako mwaka 1616 hadi mwaka 1633.

Askofu Pagano anasema, kwa mara ya kwanza, umma utapata fursa ya kujionea, kujisomea na kujichotea utajiri mkubwa unaofumbatwa katika Nyaraka za Siri za Vatican. Maendeleo ya teknolojia ya habari yatawawezesha watazamaji kuingia katika undani wa nyaraka hizi za kipapa na kufanya tathmini ya kina kuhusu mchango wake kwa maisha na utume wa Kanisa; katika masuala ya maisha, tamaduni, ujuzi na maarifa.

Mstahiki Meya wa Jiji la Roma Giovanni Alemanno anasema, Jiji la Roma linaona fahari kubwa kuweza kuwa ni mwenyeji wa onesho hili la pekee, hali inayoonesha uhusiano wa karibu kati ya Vatican na Jiji la Roma katika maisha ya kiroho na kimwili. Tukio hili ni kielelezo cha ushupavu na uwazi wa Vatican kuweza kuonesha nyaraka za Siri, nje ya kuta za Vatican. "Lux Arcana" hapo Februari, 2012, itakuwa ni fursa nyingine kwa mahujaji kujionea utajiri uliomo kwenye Nyaraka za Siri za Vatican na hija ya maisha ya mwanadamu: kiroho na kimwili.

Friday, September 23, 2011

Saturday, September 17, 2011

Seminar on entrepreneurship....What young entrepreneur has to do.

Seminar on entrepreneurship
Who Are Entrepreneurs?
Independent individuals, intensely committed and determined to continue, who work very hard.
They are confident optimists who strive for integrity.

They born with the competitive desire to excel and use failure as a learning tool.
Entrepreneurship Traits
          Imagination- is powerfully than knowledge
          Always questioning. "The important thing is not to stop questioning." One of the most important questions an entrepreneur can ask is How can I make it better?
          Instinct- intuition
          Strong positive attitude. "Weakness of attitude becomes weakness of character.“
           empathy, as in understanding how other people think and feel about things.
          Willingness to work hard, shoulder to shoulder with other people. Cliche, but true: the harder I work, the luckier I get.
          Listening carefully. Shutting up.
          Vision for what they can build. Imagining a happy future. Dreaming. Making mistakes. You have to deal with failure.
      Environmental push

Choice of Entrepreneurship is related to external factors beyond the individual’s control, seen as a “cultural phenomenon”
Culture
n  Some cultural groups see Entrepreneurship as a more desirable career opportunity. Eg Chaga
Family Background
                Entrepreneurial traits are impacted by birth order, role models and experience of rejection in childhood
n  First born: self confidence, independence and internal locus of control à correlation exists with reception of special attention & care
Marginal/Displacement Approach
Some studies show that marginal individuals are more likely to become Entrepreneurs
n  “Misfits” that cannot fit into the ‘business mainstream’
n  Dislike 9am to 5pm routine
n  Problem with acceptance of authority
n  Difficulty in coping with bureaucracy
“Ten mental locks” that can limit individual creativity. Give
          Searching for the one right answer
          Focusing on being logical
          Blindly following the rules
          Constantly being practical
          Becoming overly specialized
          Avoiding ambiguity
          Fearing looking foolish
          Fearing mistakes and failure
          Believing that “I’m not creative”
Entrepreneurship challenges in TZ
          Capital  mobilization
          Lack of entrepreneurship training
          Lack of entrepreneurship skills
          Poor government policy, regulations and laws
          Average thinking ,not extreme thinking
          Culture and beliefs
          Corruption
How did I became an entrepreneur
          By necessity
          Talk about how money works
          Employment mind set , “A”  for good jobs . What good job means to us all.
          Research your market, but don't take too long to act.
           Work for other people first and learn on their money.
           Start out slowly. Start your business when you have a customer. Maybe try your venture as a sideline first.
           Set specific objectives, but don't set your goals too high. Remember, there is no easy money.
          Plan your objectives within specific time frames.
          Surround yourself with people who are smarter than you - including an accountant and  directors who are interested in your wellbeing and who will give you straight answers.
          Don't be afraid to fail. Former football coach Vince Lombardi summarized the entrepreneurial philosophy when he said, "We didn't lose any games this season, we just ran out of time twice". New entrepreneurs must be ready to run out of time a few times before they succeed.

 ASANTENI SANA>>THANKS MUCH KWA KONGAMANO

Mlezi wa viwawa - njiro Fr. Eustaki C. Tarimo,

Mlezi wa vijana (Viwawa) wa Jimbo kuu la Arusha Sr.Immaculate Anna Joseph.

KAMATI TENDAJI YA PAROKIA YA NJIRO

FRT.PAUL RAIA POLYCARP

 Mwenyekiti wa Viwawa njiro- Nicolaus M. Venant

Mhazini wa Viwawa Njiro - Selecius E .Majegero

MAKAMU KATIBU WA VIWAWA NJIRO-JANE MAKETA

KATIBU MPYA WA VIWAWA NJIRO-FRANCISCA JOSEPH

MAKAMU MWENYEKITI VIWAWA NJIRO - EDWIN KARABA BAZIWANI.

KIONGOZI WA HAKI NA AMANI.

MHAZINI MSADIZI>>INNOCENT NA VIWAWA NJIRO

 

Friday, September 16, 2011

KONGAMANO LA TAIFA LA VIWAWA ARUSHA 2011 KTK PICHA

DHAMIRA KUU YA KONGAMANO-Tuwe na mizizi ndani ya YESU KRISTU,wakoloth 2;7,Viwawa waliwasili siku ya JUMANNE 06/09/2011.VIWAWA NA WAGENI WOTE walifika salama.
UFUNGUZI;MISA YA MISA TAKATIFU.SOMO LA KWANZA:Muhubili 11;9-12.Somo la pili Wafilipi 3;12-21,INJILI YOHANE 21;1-14-Kanisa ni letu vijana Tukaze buti tupige injili,
08.09.2011>>>Neno la kufungua kipindi Waraka wa Petro 4;5-11 MADA;MIITO NA FAMILIYA,Mr.Misago chales.

Sunday, August 14, 2011

PAROKIA YA NJIRO ARUSHA YANUNUA GARI mpya yabarikiwa leo 11.08.2011

Matukio katika picha ya Parokia ya kubariki gari yetu ya parokia leo hii........
Hawa ni Wazungu kutoka ITALY walikuja kutembelea Viwawa njiro siku ya keo ya tarehee 11.08.2011



Saturday, April 30, 2011

Catholics need to be awake to reality of evil, pope says at audience

VATICAN CITY (CNS) -- When Jesus asked his disciples to stay awake while he prayed in the Garden of Gethsemane, he was asking every believer throughout history to remain awake to the reality of God and to the reality of sin, Pope Benedict XVI said.

Jesus' request that his disciples keep watch was "a permanent message for all times because the drowsiness of his disciples was not just a problem in that moment; it is a problem throughout history," the pope said April 20.

Explaining the liturgies of Holy Week and Easter to an estimated 13,000 people gathered in St. Peter's Square, Pope Benedict said the drowsiness that Jesus warns all believers against is "a certain insensitivity of the soul to the power of evil, insensitivity to all the evil in the world; we don't want to let ourselves be too bothered by these things. We want to forget them or we try to think they aren't so serious."

But, the pope said, the lack of awareness about evil is the flip side of an equal lack of awareness about the presence and love of God.

"This is our real drowsiness," the pope said. "We don't feel God's presence, it would disturb us," so we "stay on the path of our own comfort."

"We must also stay vigilant in order to do good, to struggle on behalf of the force of goodness," Pope Benedict said.

Unlike Jesus, whose humanity allowed him to experience suffering and anguish at the thought of suffering and death, but whose obedience led him to accept God's will completely, the pope said, most people "struggle against God's will," thinking it will lead them into slavery.

 

The Holy Week and Easter liturgies, which culminate in the proclamation of Christ's resurrection, are a clear reminder that true life and freedom come from doing God's will, the pope said.

Pope Benedict prayed that Catholics everywhere would experience the Holy Week and Easter services as moments to reaffirm their own commitment to doing God's will, "aware that in doing so -- even when it seems hard and in contrast to our own desires -- we find precisely that which truly is good for us, the path to life."

Among those at the audience were more than 3,000 students from more than 200 universities participating in the Opus Dei-run UNIV conference and pilgrimage.

The pope told the students, "I hope these days in Rome will be an opportunity to rediscover the person of Christ and will give you a strong experience of church so that you can return home enlivened with a desire to witness to the mercy of the heavenly Father."

- - -

Editor's Note: The text of the pope's audience remarks in English will be posted online at: www.vatican.va/holy_father/benedict_xvi/audiences/2011/documents/hf_ben-xvi_aud_20110420_en.html.

The text of the pope's audience remarks in Spanish will be posted online at: www.vatican.va/holy_father/benedict_xvi/audiences/2011/docu
ments/hf_ben-xvi_aud_20110420_sp.html.

Monday, March 7, 2011

VIWAWA NJIRO ZIWA DULUTI .

Hapa wana Viwawa njiro siku ya jumapili ya jana (07.03.2011) wakiwa wanajianda kuanza safari ya kuelekea ziwa Duluti.na picha za chini ni matukio ya picha za ziwa Duluti.
Picha ya chini ni MHAZINI WA VIWAWA NJIRO-Selesius Majegero.
HAWA JUU NI KAMATI TENDAJI YA VIWAWA NJIRO.
PICHA NA POZI.
KAKA HAPA NI VIONGOZI WA VIWAWA NJIRO HAPO JUU.

Picha zote za hapo juu ndio muonekano wa safari ya VIWAWA njiro siku ya jana.

Monday, February 28, 2011

VIONGOZI WAPYA WA VIWAWA NJIRO

Vijana ( VIWAWA) wa parokia ya familia  takatifu njiro jana kwa kushirikiana na mlezi wao Father Austaki Tarimo walifanya uteuzi mdogo wa viongozi vijana kutokana na uongozi huo kulegalega kutokana ka kuwa na mapengo mengi.. uongozi umefikia uamuzi huo kutoka na kujiuzuru m/mwenyekiti wiki 2 tu baada ya uchaguzi, pia wamemsimamisha katibu wao kutokana na kutowajibika ipasavyo na maswala ya vijana, kulegalega kwa katibu msaidizi,lakini katibu msaidizi alipewa onyo kali na kukiri kutowajibika ipasavyo hivyo basi na kuhaidi kuajibika kama kawaida, na kuomba uongozi umsamehe kwa yaliyopita. pia uongozi umeamua kuongeza nafasi moja ambayo awali hawakuiweka ya m/mhazini, na kutokana na majukumu mengi aliyonayo mhazini  hivyo mhazini aliomba aongezewe nguvu upande wake,Na  ufuatao ni uongozi mpya wa Viwawa njiro.

   MWENTEKITI- MTAKINGILWA VENANT NICOLAUS.
   M/MSADIZI  - EDWIN KARABA BAZIAN.
 
   KATIBU- FRANCISCA JOSEPH.
   K/MSADIZI-JANE MAKETA.

  MHAZINI  MAJEGERO SELECIUS.
  M/MSADIZI-INNOCENT JOSEPH NYAMBO.

Hii ndo safu nzima ya uongozi Viwawa njiro,kuanzia siku ya jana..

Monday, January 31, 2011

KONGAMANO LA VIONGOZI WA VIJANA (VIWAWA)JIMBO KUU ARUSHA.

Viongozi wa maparokia yote ya jimbo kuu la Arusha wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza kwa misa kongamano la viongozi  lililoanza tarehe 28/1/2011 - 30/1/2011. Kikao hicho kilifanyika parokia ya moyo safi Unga LTD Kituo cha malezi. Mada kadhaa za  kuwaandaa viongozi kwa mwaka huu wa kongamano la kitaifa litakalo fanyika jimboni Arusha. yafuatayo yalijadiliwa kwenye kikao hicho ambacho ki-utaratibu kilifahamika kama kikao cha halmashauri ya vijana (VIWAWA) Jimbo kuu la Arusha. viongozi wa jimbo waalisoma  muhtasari  wa mkutano, yatokanayo,walisoma taarifa ya utekelezaji,walisoma taarifa ya fedha, Kujadili kongamano la taifa + dunia  na kuweka maazimio.  Mengi yaliyojadiliwa  pamoja na mipango pia yanahitaji zaidi maombi na sala ili yaweze kufanikishwa, kila mmoja wetu anapopanga jambo basi amtangulize Mungu. Mungu aibariki Halmashauri ya Jimbo kuu  la Arusha na mafanikio mema. ya maandalizi aaaaamen.   Mwandishi. Majegero Selecius.

Kanisa Katoliki...

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Rukia: urambazaji, tafuta
Papa Benedikto XVI, askofu wa Roma na mkuu wa Kanisa Katoliki
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
StPetersBasilicaEarlyMorning.jpg
Imani
Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo
Papa: Benedikto XVI
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki
Historia
Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi
Ibada
Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi
Mapokeo ya liturujia
Liturujia ya Kilatini (Roma Milano Lyon Toledo)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia
Jina hilo linatumika hasa kumaanisha Kanisa la Kikristo linalokubali mamlaka ya Papa wa Roma kama mkuu wa Maaskofu juu yake lote.
Kanisa hilo linaamini kuwa ndani yake linadumu moja kwa moja Kanisa pekee lililoanzishwa na Yesu Kristo ambalo wanaunganishwa nalo wote wanaobatizwa katika madhehebu yoyote. Tofauti kati yao ni kwamba baadhi (Wakatoliki) wana ushirika kamili nalo, wakati wengine (hasa Waorthodoksi na Waprotestanti) wana ushirika nalo la viwango mbalimbali, kadiri wanavyokubali mafundisho, sakramenti na uongozi wake.
Neno "katoliki" linatokana na kivumishi cha Kigiriki καθολικός (katholikòs), lenye maana ya «kamili, kadiri ya utimilifu». Kwa mara ya kwanza liliandikwa na Ignas wa Antiokia kwa Wakristo wa Smirna mwanzoni mwa karne II: «Alipo Yesu Kristo ndipo lilipo Kanisa Katoliki» (Ad Smyrnaeos, 8).
Kati ya madhehebu ya Kikristo, Kanisa Katoliki linakusanya waamini 1,147,000,000, yaani nusu ya wafuasi wote wa Yesu, na 17.3 % ya binadamu wote, likiwa na asilimia kubwa ya waamini kati ya wananchi wa Amerika na Ulaya.
Kanisa Katoliki linaishi katika majimbo karibu 3,000, ambayo kwa kawaida yanaongozwa na Maaskofu wakisaidiwa na mapadri na mashemasi; kati ya hayo, mengi yanafuata mapokeo ya magharibi, lakini machache mapokeo ya mashariki. Majimbo yanagawanyika katika parokia zinazoongozwa na padri anayeitwa paroko.
Kati ya waamini wana nafasi ya pekee wamonaki na watawa wengine ambao wanaishi kwa mitindo iliyostawi katika historia ya Kanisa ili kumfuata Yesu kwa karibu zaidi katika useja mtakatifu, ufukara na utiifu.

MOTO WA KATIBA MPYA WAZIDI KUSHIKA KASI, KANISA KATOLIKI WAJITOSA

HATIMAYE Kanisa Katoliki nchini limejitosa rasmi katika mjadala wa katiba mpya likisema kuwa linaunga mkono mchakato huo, lakini likihadharisha kuwa mchakato huo unahitaji subira, weledi na ujasiri wa kisiasa kukubali mabadiliko.

Hayo yamo katika tamko maalumu lililotolewa na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) katika mkutano usiokuwa wa kawaida uliofanyika jijini Mwanza kuanzia Januari 10-11, mwaka huu na  kusainiwa na Rais wa baraza hilo Jude Thaddaus Ruwa’ichi.

Maaskofu wa kanisa hilo pamoja na mambo mengine walizungumzia suala la katiba mpya na tukio la kitaifa la maadhimisho ya Jubilei ya miaka 50 ya uhuru wa nchi.

Kanisa hilo lilitoa wito kwa serikali na wadau wote kujadili mchakato huo wa kuandika katiba mpya likitaka busara itumike ili kufuata mchakato uliowazi wakati wa kuiandaa.

“Tunamshukuru, kwanza Rais amelitambua hilo na hivyo amekubali na kudhamiria kuhakikisha kwamba nchi yetu inakuwa na utaratibu mzuri wa kuratibu mambo yake kwa njia ya katiba inayoendana na wakati,” lilisema kanisa hilo kupitia tamko hilo maalumu na kuongeza.

“Ni matarajio yetu kwamba ili kufikia lengo na matamanio ya Watanzania walio wengi ya kuwa na katiba inayoendana na wakati, yenye misingi imara ya kidemokrasia na inayobeba matumaini ya Watanzania kuelekea miaka 50 ijayo, busara itatumika ili kufuata mchakato uliowazi.”

Kanisa lilifafanua kuwa katika kutumia busara huko kutafanya mchakato huo kuwa wazi wa  haki na unaokubalika na wengi na kwamba utawezesha  kupatikana kwa  katiba inayolinda tunu za taifa ambazo ni amani umoja mshikamano  na pia maslahi ya Watanzania wote.

Kanisa limeshauri uwapo wa jitihada za makusudi za kushirikisha watu wengi kutoka makundi mbalimbali yatakayochangia kupata mwafaka wa kitaifa juu ya katiba gani wanayoitaka Watanzania.

“Kwa kuwa bunge ni chombo cha wawakilishi wa nchini vema chombo hiki kikishirikishwa tangu mwanzo hasa katika kuweka taratibu za kufanikisha shughuli hiyo na mwisho kupata ridhaa kwa wananchi wote (referendum), mchakato huu utahitaji weledi, subira, uvumilivu wa kisiasa na ujasili wa kukubali mabadiliko,” inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Katika tarifa hiyo maaskofu waliweka bayana kuwa wao wanaunga mkono na kwamba wanatia moyo mchakato huo na na kuwaalika Watanzania wote kuungana pamoja kuliombea taifa liweze kudumu katika upendo uelewano umoja na amani.

Kuhusu maadhimisho ya Jubilie ya miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara kanisa limeelekeza waumini wake kushiriki kikamilifu katika sherehe hizo kwa kusali sala maalumu ya kuliombea taifa kuanzia ngazi ya Jumuiya, Parokia na Jimbo.

“Wazo  ama lengo kuu la Kanisa Katoliki kusherehekea Jubilei ya Uhuru wa Tanzania ni kumshukuru Mungu na kuona kwamba uhuru tulioupata unaendelea kuwasaidia watu kuishi kama wana wa Mungu, maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania pia yamelenga kuongeza uelewa wa waumini na Watanzania wote juu ya umuhimu wa uhuru wa watu na taifa,” lilisema.

Sababu nyingine ni kutathmini mafanikio, matatizo, na changamoto muhimu za kitaifa za kanisa katoliki katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru katika kumwendeleza  Mtanzania kiroho na kimwili na kuweka malengo ya jumla ya kudumisha uhuru wa Taifa la Tanzania.

Katika kuhakikisha kanisa linashiriki kikamilifu katika maadhimisho hayo, limeziagiza mamlaka zake za chini kuanzia ngazi ya jumuiya, kigango na Parokia kusali sala maalumu kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania bara kila zinapokutana na kuimba wimbo wa taifa pale inapobidi kufanya hivyo.

“Ili kufanikisha hilo, pamoja na mambo mengine , tunapendekeza kwamba kadiri ya nafasi na mazingira, wimbo wetu wa Taifa uimbwe mara kwa mara kadiri iwezekanavyo katika ibada zetu kama vile katika misa za Jumapili na katika shughuli zingine za kikanisa”, lilisema tamko.

Pia imeelezwa kuwa Parokia na Jimbo zitatakiwa  kutenga siku maalum kwa ajili ya kuadhimisha misa maalumu kwa nia ya kumshukuru Mungu kwa kufikisha miaka 50 ya uhuru na kuliombea Taifa liweze kudumu katika upendo, amani umoja na mshikamano.

“Misa hizi ziadhimishwe kwa kufuata mtiririko kulingana na Kalenda ya litrujia, iteuliwe siku moja kwa ajili ya Misa ya Parokia, misa hii ifanyike Mei 31 na Agosti 15 , Misa ya Jimbo na ile ya kitaifa itafanyika karibu na kilele cha Sherehe za Uhuru  (Desemba 9  mwaka huu,” lilisema kanisa hilo.

Kanisa  hilo lilifafanua kuwa katika sherehe hizo kutakuwa na harakati za kuwahamasisha Wakristo na Watanzania kwa ujumla juu ya umuhimu wa uhuru katika kujipatia maendeleo ya kiroho na kimwili.

Aidha kanisa hilo  limeitisha kongomano la kitaifa litakalofanyika Novemba 11 na 12 mwaka huu, lengo likiwa kutoa fursa kwa waumini na watu wote kutafakari juu ya wapi wametoka, walipo na wanakotaka kwenda kama taifa.

Moto wa kudai katiba mpya, uliwashwa na Chadema Novemba mwaka jana, baada ya kutangaza kutotambua kura zilizomweka madarakani Rais Jakaya  Kikwete. Kutokana na hali hiyo, chama hicho kilianza mchakato wa kushikiza kuundwa kwa katiba mpya kwa kususia hotuba ya Rais Kikwete wakati wa akizindua Bunge la 10.

Pia wabunge pamoja na viongozi wa chama hicho walisusia sherehe za kuapishwa kwa Rais.
Katika kuendeleza madai hayo, hivi karibuni mbunge wa Jimbo la Ubungo kupitia Chadema, John Mnyika aliwasilisha hoja binafsi kwenye Ofisi za Bunge, hoja iliyokuwa na lengo la kudai katiba mpya.

Nao Wanachama wa CUF,  hivi karibuni walifanya maandamano ya kuwasilisha rasimu ya katiba mpya kwa Waziri wa Katiba na Sheria. Pia viongozi mbalimbali wastaafu, walipo madarakani wamekuwa wakieleza umuhimu wa kuwa na Katiba mpya.

Miongoni mwa waliojitokeza adharani na kuunga mkono uwepo wa katiba mpya ni pamoja na Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, Mawaziri Wakuu wa zamani, Joseph Warioba na Frederick Sumaye, Jaji Mkuu Mstaafu na Augustino Ramadhani, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Jaji Omar Makungu pamoja na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ambaye aliahidi kumshauri Rais juu ya suala la kuundwa kwa Katiba mpya.

Madai ya Katiba mpya pia yamewahi kutolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa ambaye alisema bayana kuwa katiba mpya iandikwe mapema kabla ya mambo kuwa mabaya, akitoa mfano wa mapungufu ya katiba ya sasa kuwa ni rais kupewa madaraka makubwa.

Lakini akiwa Ikulu kwenye hafla ya kuapishwa Jaji Mkuu Mpya, Mohamed Othman Chande, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) Frederick Werema, alisema kuwa haoni haja ya kuandikwa katiba mpya badala yake katiba iliyopo, iwekewe viraka.

“Kuandika Katiba mpya hapana, lakini kufanya marekebisho kwa kuondoa au kuongeza mambo fulani kwenye katiba, ruksa,” alisema Jaji Werema.