Monday, January 31, 2011

KONGAMANO LA VIONGOZI WA VIJANA (VIWAWA)JIMBO KUU ARUSHA.

Viongozi wa maparokia yote ya jimbo kuu la Arusha wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza kwa misa kongamano la viongozi  lililoanza tarehe 28/1/2011 - 30/1/2011. Kikao hicho kilifanyika parokia ya moyo safi Unga LTD Kituo cha malezi. Mada kadhaa za  kuwaandaa viongozi kwa mwaka huu wa kongamano la kitaifa litakalo fanyika jimboni Arusha. yafuatayo yalijadiliwa kwenye kikao hicho ambacho ki-utaratibu kilifahamika kama kikao cha halmashauri ya vijana (VIWAWA) Jimbo kuu la Arusha. viongozi wa jimbo waalisoma  muhtasari  wa mkutano, yatokanayo,walisoma taarifa ya utekelezaji,walisoma taarifa ya fedha, Kujadili kongamano la taifa + dunia  na kuweka maazimio.  Mengi yaliyojadiliwa  pamoja na mipango pia yanahitaji zaidi maombi na sala ili yaweze kufanikishwa, kila mmoja wetu anapopanga jambo basi amtangulize Mungu. Mungu aibariki Halmashauri ya Jimbo kuu  la Arusha na mafanikio mema. ya maandalizi aaaaamen.   Mwandishi. Majegero Selecius.

No comments:

Post a Comment