Monday, January 31, 2011

Kanisa Katoliki...

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Rukia: urambazaji, tafuta
Papa Benedikto XVI, askofu wa Roma na mkuu wa Kanisa Katoliki
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
StPetersBasilicaEarlyMorning.jpg
Imani
Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo
Papa: Benedikto XVI
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki
Historia
Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi
Ibada
Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi
Mapokeo ya liturujia
Liturujia ya Kilatini (Roma Milano Lyon Toledo)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia
Jina hilo linatumika hasa kumaanisha Kanisa la Kikristo linalokubali mamlaka ya Papa wa Roma kama mkuu wa Maaskofu juu yake lote.
Kanisa hilo linaamini kuwa ndani yake linadumu moja kwa moja Kanisa pekee lililoanzishwa na Yesu Kristo ambalo wanaunganishwa nalo wote wanaobatizwa katika madhehebu yoyote. Tofauti kati yao ni kwamba baadhi (Wakatoliki) wana ushirika kamili nalo, wakati wengine (hasa Waorthodoksi na Waprotestanti) wana ushirika nalo la viwango mbalimbali, kadiri wanavyokubali mafundisho, sakramenti na uongozi wake.
Neno "katoliki" linatokana na kivumishi cha Kigiriki καθολικός (katholikòs), lenye maana ya «kamili, kadiri ya utimilifu». Kwa mara ya kwanza liliandikwa na Ignas wa Antiokia kwa Wakristo wa Smirna mwanzoni mwa karne II: «Alipo Yesu Kristo ndipo lilipo Kanisa Katoliki» (Ad Smyrnaeos, 8).
Kati ya madhehebu ya Kikristo, Kanisa Katoliki linakusanya waamini 1,147,000,000, yaani nusu ya wafuasi wote wa Yesu, na 17.3 % ya binadamu wote, likiwa na asilimia kubwa ya waamini kati ya wananchi wa Amerika na Ulaya.
Kanisa Katoliki linaishi katika majimbo karibu 3,000, ambayo kwa kawaida yanaongozwa na Maaskofu wakisaidiwa na mapadri na mashemasi; kati ya hayo, mengi yanafuata mapokeo ya magharibi, lakini machache mapokeo ya mashariki. Majimbo yanagawanyika katika parokia zinazoongozwa na padri anayeitwa paroko.
Kati ya waamini wana nafasi ya pekee wamonaki na watawa wengine ambao wanaishi kwa mitindo iliyostawi katika historia ya Kanisa ili kumfuata Yesu kwa karibu zaidi katika useja mtakatifu, ufukara na utiifu.

No comments:

Post a Comment